Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, September 18, 2013

Waasi wa Boko Haram waua wanajeshi 40 Nigeria


Waasi wa Boko Haram waua wanajeshi 40 Nigeria
Wanajeshi wa Nigeria wasiopungua 40 wameuliwa na wengine 65 hawajulikani waliko katika mapambano kati yao na wanamgambo wanaoaminika kuwa wa kundi la Boko Haram. Mapigano hayo yalitokea Ijumaa iliyopita katika barabara ya Baga-Maiduguri  kaskazini mashariki mwa Nigeria. Uchunguzi umeanza ili kujua sababu ya kushindwa oparesheni hiyo iliyopelekea kuuliwa wanajeshi wengi wa Nigeria. Afisa wa jeshi la Nigeria aliyesimamia oparesheni hiyo maalumu dhidi ya wanamgambo wa kundi la Boko Haram amefutwa kazi kufuatia kuuliwa wanajeshi wengi. Jumapili iliyopita pia wanamgambo wanne wa Boko Haram waliuliwa na kikosi cha oparesheni cha kiraia katika mji wa Mubi katika jimbo la Adamawa huko mashariki mwa Nigeria. 

No comments:

Post a Comment