skip to main |
skip to sidebar
Obama ashindwa kupata uungaji mkono Marekani
Uchunguzi mpya wa maoni huko Marekani unaonyesha kushindwa Rais
Barack Obama wa nchi hiyo katika kupata uungaji mkono wa raia wa nchi
hiyo kuhusiana na suala la kuivamia kijeshi Syria. Uchunguzi mpya wa
maoni uliofanywa na shirika la habari ya Reuters na shirika la utafiti
la Ibson huko Marekani unaonyesha kuwa Rais Barack Obama ameshindwa
kuwashawishi Wamarekani kupitia mahojiano aliyofanya kwa njia ya
televisheni ili wamuunge mkono katika mashambulizi dhidi ya Syria.
Kw amujibu wa matokeo ya uchunguzi huo wa maoni uliofanyika wiki
iliyopita huko Marekani, theluthi tatu ya Wamarekani wanasisitiza
kutatuliwa mgogoro wa Syria kupitia makubaliano ya kimataifa. Aidha
uchunguzi huo wa maoni umeonyesha kuwa, asilimia 25 tu ya raia wa
Marekani wanapinga kutatuliwa mgogoro wa Syria kwa njia za kidiplomasia.
No comments:
Post a Comment