Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Saturday, September 14, 2013

Obama ashindwa kupata uungaji mkono Marekani


Obama ashindwa kupata uungaji mkono MarekaniUchunguzi mpya wa maoni huko Marekani unaonyesha kushindwa Rais Barack Obama wa nchi hiyo katika kupata uungaji mkono wa raia wa nchi hiyo kuhusiana na suala la kuivamia kijeshi Syria. Uchunguzi mpya wa maoni uliofanywa na shirika la habari ya Reuters na shirika la utafiti la Ibson huko Marekani unaonyesha kuwa Rais Barack Obama ameshindwa kuwashawishi Wamarekani kupitia mahojiano aliyofanya kwa njia ya televisheni ili wamuunge mkono katika mashambulizi dhidi ya Syria.
Kw amujibu wa matokeo ya uchunguzi huo wa maoni uliofanyika wiki iliyopita huko Marekani, theluthi tatu ya Wamarekani wanasisitiza kutatuliwa mgogoro wa Syria kupitia makubaliano ya kimataifa. Aidha uchunguzi huo wa maoni umeonyesha kuwa, asilimia 25 tu ya raia wa Marekani wanapinga kutatuliwa mgogoro wa Syria kwa njia za kidiplomasia.

No comments:

Post a Comment