Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 3, 2013

Wapalestina watungua ndege ya kijasusi ya Israel


Wapalestina watungua ndege ya kijasusi ya Israel
Wanamapambano wa Palestina katika Ukanda wa Ghaza wamefanikiwa kuitungua ndege ya kijasusi ya utawala wa Kizayuni katika anga ya ukanda huo na kuiteka.
Televisheni ya al Mayadin imeripoti habari hiyo na kuongeza kuwa, vikosi vya wanamapambano wa Palestina katika Uganda wa Ghaza, vimefanikiwa kuitungua ndege ya kijasusi ya utawala wa Kizayuni katika anga ya kaskazini mwa Ukanda wa Ghaza na kuiteka.
Viongozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamethibitisha habari ya kuanguka ndege hiyo na kudai kuwa haikutunguliwa, bali imeanguka kutokana na matatizo ya kiufundi. Itakumbukwa kuwa juzi Ijumaa, jeshi la utawala wa Kizayuni liliwaua shahidi Wapalestina wanne kaskazini mwa Ghaza na kuwajeruhi wengine kadhaa. Wanamapambano wa Palestina hao walijibu mashambulizi hayo na kujeruhi wanajeshi kadhaa vamizi wa utawala wa Kizayuni.
Israel inadai kuwa, shambulizi la kifaru cha utawala huo liliwalenga wapiganaji wa Brigedi za Izzuddin Qassam, tawi la kijeshi la HAMAS hata hivyo watu walioshuhudia walisema kuwa shambulio hilo lililenga nyumba za wakulima wa Kipalestina. Maafisa wa Hamas kwa upande wao walisema helikopta moja ya Israel aidha ilivurumisha maroketi kadhaa kwenye eneo hilo.

No comments:

Post a Comment