Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, November 20, 2013

OIC yaunga mkono natija ya kikao cha Kuwait


OIC yaunga mkono natija ya kikao cha KuwaitNaibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) amesema kuwa jumuia hiyo inaunga mkono maamuzi na maazimio yaliyofikiwa katika kikao cha wakuu wa nchi za Kiarabu na Kiafrika huko Kuwait. Samir Bakr Diab ameeleza kuwa OIC inaunga mkono maamuzi na maazimio yaliyofikiwa katika kikao hicho cha Kuwait khususan katika uwanja wa mapatano ya kibiashara kati ya nchi za Kiarabu na Kiafrika na kuondolewa vizuizi vilivyopo katika uwanja huo.
Akizungumza katika kikao cha tatu cha wakuu wa nchi za Kiarabu na Kiafrika huko Kuwait kwa niaba ya Ikmaluddin Ehsanoghlo Katibu Mkuu wa OIC, Naibu Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo Samir Bakr Diab amesema kuwa taasisi hiyo imeanzisha mfuko wa maendeleo ya mshikamano wa Kiislamu wenye mtaji wa dola bilioni kumi ili kuzisaidia taasisi mbalimbali za kibiashara za nchi wanachama wa jumuiya hiyo.  

No comments:

Post a Comment