Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 3, 2013

Mufti wa Libya aonya kuhusu kugawika nchi hiyo


Mufti wa Libya aonya kuhusu kugawika nchi hiyoMufti wa Libya ametahadharisha kuhusu suala la kuifanya nchi hiyo kuwa shirikisho katika mazingira yasiyoridhisha ya hivi sasa. Sheikh Sadiq al Ghiryani amesema kuwa, moja ya malengo ya mapinduzi ya Februari 17 nchini humo lilikuwa ni kulinda umoja wa kitaifa wa Libya na kueleza kuwa hali ya mambo ya hivi sasa ya Libya hairidhishi, hivyo suala la kutaka kuifanya Libya kuwa shirikisho linalenga kuigawa vipande vipande nchi hiyo.
Mufti huyo wa Libya amesema, kitendo cha serikali ya Tripoli cha kutowajali wananchi, kimetoa msukumo kwa raia hao kutoa ombi hilo la kutaka kuifanya Libya kuwa shirikisho. Ameongeza kuwa viongozi wa serikali wanapasa kuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yao ili kuzuia kukiukwa umoja wa mamlaka ya nchi. Wakati huohuo umoja wa maulamaa wa Libya  pia umesema kuwa, kuifanya Libya kuwa shirikisho ni kitendo haramu na marufuku na kusisitiza kuwa mfumo wa shirikisho una madhara makubwa kwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment