Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, November 20, 2013

Sultani Makenga kupewa hifadhi nchini Uganda


Sultani Makenga kupewa hifadhi nchini Uganda
Afisa mmoja wa vyombo vya usalama vya Uganda amearifu kuwa Sultani Makenga mmoja wa makamanda wa waasi wa M23 aliyekimbilia nchini humo atapewa hifadhi. Afisa huyo ameeleza kwamba, kamanda huyo alikimbilia Uganda baada ya kushindwa waasi hao huko mashariki mwa Kongo na kwamba kwa sasa anashikiliwa na jeshi la UPDF. Ameongeza kuwa, kutokana na sababu za kiuslama serikali ya Kampala haitotangaza mahali alipo Sultani Makenga. Makenga anatuhumiwa na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kufanya jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu.
Serikali ya Kampala imetangaza kuwa waasi 1,000 wameingia nchini humo kupitia mipaka ya magharibi mwa Uganda baada ya kushindwa katika mapigano na vikosi vya Kongo vilivyokuwa vikisaidiwa na askari wa Umoja wa Mataifa. Uganda inayotuhumiwa na Kongo kuwaunga mkono waasi wa M23 imesema kuwa, haiko tayari kuwarejesha nyumbani waasi hao.

No comments:

Post a Comment