Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 3, 2013

US kuipa Iraq zana za kijeshi kukabiliana na magaidi


US kuipa Iraq zana za kijeshi kukabiliana na magaidiRais Barack Obama wa Marekani na Nouri al Maliki Waziri Mkuu wa Iraq wamekubaliana juu ya mpango wa Washington wa kuipatia serikali ya Baghdad zana za kisasa za kijeshi kwa shabaha ya kukabiliana na makundi ya kigaidi nchini humo. Mara baada ya kumalizika mazungumzo kati ya viongozi hao wawili katika Ikulu ya White House, Rais Obama alimuhakikishia al Maliki kwamba Washington itaipatia Iraq zana za kijeshi kwa lengo la kukabiliana na makundi ya kigaidi ambayo yamekuwa yakiendesha operesheni za kigaidi kila kona ya nchi hiyo. Kwenye mazungumzo hayo, naye Waziri Mkuu wa Iraq amesema kuwa, demokrasia nchini Iraq inalegalega, ingawa serikali inafanya juhudi za kuondoa kasoro na hitilafu zilizopo. Kabla ya kuelekea Marekani, siku ya Jumanne iliyopita Nouri al Maliki alisikika akisema kuwa, makundi ya kigaidi kutoka nje ya nchi hiyo yameingia nchini Iraq kwa shabaha ya kufanya ghasia na machafuko nchini humo.

No comments:

Post a Comment