Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, November 19, 2013

Arab League yalaani machafuko nchini Libya


Arab League yalaani machafuko nchini Libya
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) amelaani vikali vitendo vya ukatili vilivyotokea Tripoli, mji mkuu wa Libya dhidi ya waandamanaji wasio na silaha. Mbali na Nabil al-Arab kulaani machafuko hayo ya hivi karibuni ya mjini Tripoli ambapo makumi ya waandamanaji waliuliwa na kujeruhiwa, amezitaka pande zote kuunga mkono juhudi za serikali na baraza la kongresi ya kitaifa nchini humo za kuikwamua nchi hiyo na hali mbaya iliyo nayo hivi sasa. Aidha al-Arab ameonyesha kusikitishwa kwake na matukio hayo na akaongeza kuwa, vitendo vya utumiaji mabavu nchini Libya vimefikia kiwango cha kutisha. Hii ni katika hali ambayo jana baadhi ya duru za habari ziliripoti kujiri mapigano yaliyowahusisha wakazi wa eneo la al-Shawkh huko Swalahu al-Din katika viunga vya mji mkuu Tripoli, na wanamgambo wenye silaha. Watu 47 waliuawa na wengine 500 kujeruhiwa baada ya makundi ya watu wenye silaha kuwamiminia risasi waandamanaji waliokuwa wakipinga vitendo vya utumiaji mabavu nchini humo.

No comments:

Post a Comment