Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, November 19, 2013

Wanawake wa Ikhwan Muslimin kizimbani Misri


Wanawake wa Ikhwan Muslimin kizimbani MisriDuru za habari nchini Misri zimeripoti kuwa, kwa akali wanawake 15 na wasichana 7 wenye mahusiano na kundi la Ikhwanul Muslimiin, wanatazamiwa kupandishwa kizimbani, kwa tuhuma za kuhusika na vitendo vya kikatili katika maandamano yaliyopita nchini humo. Habari zinasema kuwa wanachama hao watapandishwa kizimbazi hapo kesho. Ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu nchini Misri imetangaza kuwa, itawafikisha mahakamani wanawake hao ambao pia wanatajwa kuwa miongoni mwa wafuasi wa rais aliyeuzuliwa madarakani, Muhammad Mursi, kesho Jumatano, Novemba 20, ili kujibu tuhuma dhidi yao. Ripoti hiyo imeongeza kuwa, wanawake hao walitiwa nguvuni mwishoni mwa mwezi uliopita wakituhumiwa kuhusika na machafuko yaliyotokea katika eneo la Rushdi mkoani Alexandria. Wasichana 7 kati ya watuhumiwa hao wanatajwa kuwa na umri kati ya miaka 18 na kuendelea na kwamba, wanaendelea kushikiliwa na vyombo vya dola nchini Misri.

No comments:

Post a Comment