
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameeleza kusikitishwa na kuuliwa shahidi na kujeruhiwa raia kadhaa wa Lebanon na wa nchi za nje katika mashambulizi hayo ya kigaidi na kutoa mkono wa pole kwa familia za wahanga wa mashambulizi hayo. Bi Afkham ameongeza kuwa kwa kuzingatia kwamba mripuko huo umetokea karibu na ubalozi wa Iran huko Beirut, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran inafuatilia suala hilo kwa makini na kwa juhudi maalumu na kwamba itatoa taarifa kamili katika uwanja huo. Watu wasiopungua 26 wameuliwa na wengine 150 kujeruhiwa katika mripuko huo.
Wakati huo huo mkuu wa idara ya utamaduni katika ubalozi wa Iran mjini Beirut Sheikh Ibrahim Ansari ameuawa shahidi katika mripuko huo. Habari hiyo imethibitishwa na kaimu waziri wa afya nchini Lebanon.
No comments:
Post a Comment