Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Tuesday, November 19, 2013

'Hujuma ya kigaidi ya Beirut ni njama za Wazayuni'


'Hujuma ya kigaidi ya Beirut ni njama za Wazayuni'Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa mashambulizi ya kigaidi yaliyotokea mkabala na ubalozi wa Iran huko Beirut mji mkuu wa Lebanon ni njama za Wazyuni na vibaraka wao. Bi Marzieh Afkham amelaani mashambulizi hayo ya kigaidi yaliyotokea leo asubuhi huko Beirut mkabala na ubalozi wa Iran mjini humo na kusisitiza kuwa, jinai hiyo ni kitendo cha chuki na uadui kilichofanywa na Wazayuni na vibaraka wao.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameeleza kusikitishwa na kuuliwa shahidi na kujeruhiwa raia kadhaa wa Lebanon na wa nchi za nje katika mashambulizi hayo ya kigaidi na kutoa mkono wa pole kwa familia za wahanga wa mashambulizi hayo. Bi Afkham ameongeza kuwa kwa kuzingatia kwamba mripuko huo umetokea karibu na ubalozi wa Iran huko Beirut, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran inafuatilia suala hilo kwa makini na kwa juhudi maalumu na kwamba itatoa taarifa kamili katika uwanja huo. Watu wasiopungua 26 wameuliwa na wengine 150 kujeruhiwa katika mripuko huo.
Wakati huo huo mkuu wa idara ya utamaduni katika ubalozi wa Iran mjini Beirut Sheikh Ibrahim Ansari ameuawa shahidi katika mripuko huo. Habari hiyo imethibitishwa na kaimu waziri wa afya nchini Lebanon.

No comments:

Post a Comment