Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Sunday, November 3, 2013

UN yalaani kupigwa vita Waislamu Myanmar


UN yalaani kupigwa vita Waislamu Myanmar
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa anayefuatilia masuala ya haki za binadamu nchini Myanmar amesema kuwa fujo na ghasia dhidi ya Waislamu zinatishia mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi nchini humo. Tomas Ojea Quintana amesema kuwa, kuendelea kushambuliwa na kutengwa Waislamu wa kabila la Rohingya katika jimbo la Rakhine kunaisawiri na kutoa picha mbaya kwa nchi hiyo na kunaitumbukiza katika hatari ya kuzuka vita vikubwa vya kidini katika miaka ijayo. Quintana amesema inasikitisha kuona kuwa, hata maafisa wa usalama pia wamejihusisha na vitendo vya manyanyaso dhidi ya Waislamu na baya zaidi ni kwamba serikali imekaa kimya bila ya kuchukua hatua zozote dhidi ya maafisa wake. Mjumbe huyo wa UN amesema hayo mbele ya kamati ya Baraza Kuu la umoja huo inayoendelea kupokea ripoti za hali ya haki za binadamu duniani.

No comments:

Post a Comment