Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, November 18, 2013

Wahamiaji haramu 61 wakamatwa Italia


Wahamiaji haramu 61 wakamatwa Italia
Maafisa wa Italia wamewatia nguvuni wahamiaji haramu 61 katika kisiwa cha kusini mwa nchi hiyo. Kikosi cha ulinzi cha pwani ya Italia leo Jumatatu kimewatia mbaroni wahamiaji haramu 61 waliokuwa na lengo la kuingia katika kisiwa cha Lampedusa kusini mwa nchi hiyo. Kisiwa cha Lampedusa kinachopatikana kati ya kisiwa cha Sicily na Tunisia hutumiwa na makumi ya wahamiaji haramu  kutoka kaskazini mwa Afrika na eneo la Mashariki ya Kati kama njia ya kufika nchini Italia na katika nchi nyingine za Ulaya.
Wahamiaji haramu zaidi ya elfu 36 mwaka huu wameingia Italia wakitafuta hifadhi.

No comments:

Post a Comment