Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Monday, November 18, 2013

Wamisri wachoma moto picha za Erdogan na Qatar



Wamisri wachoma moto picha za Erdogan na Qatar
Waandamanaji wanaomuunga mkono Abdulfatah al Sisi, Waziri wa Ulinzi wa Misri wamezichoma moto picha za Waziri Mkuu wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan na bendera ya nchi ya Qatar mjini Cairo, Misri. Waandamanaji hao waliokuwa wamekusanyika mbele ya ubalozi wa Uturuki mjini Cairo, wametaka pia kufukuzwa balozi wa Uturuki nchini kwao. Kabla ya hapo na katika kulalamikia matamshi ya viongozi wa Ankara, Cairo ilimuita balozi wa Uturuki nchini humo Hussein Own Butsali sambamba na kumuondoa balozi wake mjini Ankara. Mbali na hapo serikali ya Cairo ilitangaza kuwa, itachunguza uhusiano wake na Uturuki lakini ikatangaza kuwa, katika hali ya sasa haitamrejesha balozi wake nchini Uturuki. Nivyema kuashiria hapa kuwa, baada ya kuuzuliwa madarakani rais Muhammad Mursi wa Misri, Uturuki ambayo ilikuwa mmoja wa wakosoaji wakubwa wa hatua hiyo, ilitangazi wazi wazi kwamba, inamtambua Mursi kuwa ndiye rais pekee wa kisheria wa nchi hiyo. Aidha mbali na hapo Ankara iliendelea kulaani hatua ya kuwekwa kizuizini mteja wao huyo sanjari na kusisitiza kutaka kurejeshwa kwake madarakani nchini Misri, suala ambalo lilizidi kupigilia msumari wa moto kwenye siasa za nchi mbili. Inasemekana pia kwamba, Qatar ambayo ni muungaji mkubwa wa Harakati ya Ikhwanul Muslimiin nchini Misri, ilikata misaada yake ya kifedha kwa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika baada ya kung’olewa madarakani rais Muhammad Mursi.

No comments:

Post a Comment