Social Icons

rss feed facebook twitter google plus linkedin youtube email

Wednesday, November 20, 2013

Mugabe asema Zimbabwe si koloni la Uingereza


Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe 
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amesema kuwa, nchi ya Zimbabwe si koloni la Uingereza. Akiwahutubia wanachuo wa vyuo vikuu katika mji Mkuu Harare hapo jana, Mugabe alieleza kuwa wananchi wa Zimbabwe ijapokuwa wanazungumza vizuri na kwa ufasaha lugha ya Kiingereza lakini hawakoloniwi tena na Waingereza.
Huku akiwabeza wazungu na wakoloni wa zamani wa nchi hiyo Mugabe amesema kwamba, hawapaswi kuwapumbaza wananchi wa Zimbabwe ili kwa njia hiyo waweze kupora kikamilifu utajiri wa nchi hiyo. Aidha  sambamba na kueleza kuwa utamaduni wa kikoloni wa nchi za Magharibi umeingiza tamaduni za nje katika bara la Afrika Mugabe ameongeza kuwa, wazawa wa bara la Afrika wanatambua haki zao na kwamba wanastafidi vyema na mali asili na utajiri wao ambao kwa karne nyingi umekuwa ukiporwa na wakoloni.

No comments:

Post a Comment